Sunday, January 27, 2013

MANGULA AWALAMBISHA FAITH CHOIR MILIONI 15

Na Solomon Lekui

Makamu mwenyekiti wa CCM taifa ndugu Philip Mangula akiongozwa na mwenyekiti wa bodi ya Chuo kikuu cha Tumaini kuingia katika ukumbi wa Multipurpose kwa ajili ya kuchangia kwaya ya faith ya CCT kwa ajili ya kurekodi mkanda wa Video wa nyimbo za injili


mgeni rasmi akiwa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa iringa ndugu Jesca msambatavangu (kushoto) na mbunge wa viti maalum ndugu rita kabati na viongozi wengine wa CCM wilaya na mkoa


waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi wa Tumaini Nelly Henericus naye alikuwepo kwa ajili ya kuinua kazi ya Mungu


DPAA Dr. Richard Lubawa pamoja na DPA Dr.. Chachage wakiwa katika harambee hiyo kwa ajili ya kuichangia kwaya ya Faith CCT chuoni Tumaini


wanakwaya wakiingia jukwaani kwa mbwembwe. Utaipenda


kinadada nao hawapo nyuma kwa mapozi na tabasamu murua kabisa


kama ni dereva wa gari basi ndio huyu ambaye ni dereva (mwalimu) wa kwaya ya Faith CCT katika chuo kikuu cha Tumaini


Faith wakifanya mambo jukwaani


wageni wakitazama kwa tabasamu na furaha kwaya ya Faith wakifanya vitu vyao jukwaani


Sololist hao!!!!


Mwenyekiti wa bodi ya chuo kikuu cha Tumaini Dr. Owdenburg Mdegela ambaye pia ni askofu wa dayosisi ya Iringa akimkaribisha mgeni rasmi katika harambe hiyo


Mgeni rasmi akiwahutubia wageni waliokuwepo katika harambee hiyo


karibu mwanakwaya mwenzangu!!!! Hivyo ndivyo askofu alivyomkaribisha mgeni rasmi kuhutubia na kuchangia kwaya tayari kwa ajili ya kurekodi


Katibu wa kwaya akisoma risala fupi kwa mgeni rasmi


baada ya harambe ni hoihoi vifijo na nderemo. utaipenda tu
Makamu mwenyekiti wa CCM taifa ndugu Philip Mangula, ameongoza harambee ya kuchangia kwaya ya Faith ya CCT ya chuo kikuu cha Tumaini fedha kwa ajili ya kurekodi nyimbo zao za injili za video. Mangula aliwaambia wanakwaya kuwa alikuwa mwimbaji wa kwaya akiwa kijana na walikuwa wakitumia chombo cha kitamaduni kiitwacho Mangala kwa ajili ya kumsifu mungu wao wakiwa pamoja na askofu Mdegella

katika ukumbi huo wa Multiurpose Mangula aliwaambia washiriki kuwa ameingia kwenye siasa pasipo kusudio baada ya kuitwa na REO mwaka 1966 ili akasomee uongozi katika chuo cha uongozi kivukoni baada ya aliyechaguliwa kwenda kusoma chuo hicho kuuguliwa,ndipo alipoteuliwa kwenda kusoma hapo. Mangula alipamba ukumbi kwa kuimba wimbo wa  "Tumshukuru mungu" wimbo ambao ulipokewa kwa shangwe na waliohudhuria hapo


Katika harambee hiyo iliyojawa na viongozi wa CCM wa ngazi mbalimbali, Mh. Mangula alichangia shilingi milioni Tano,watoto wake walichangia laki saba na wadau mbalimbali wakiongozwa na mwenyekiti wa CCM mkoa ndugu Jesca Msambatavangu aliyechangia shilingi laki tano.


Takriban shilingi milioni 15 zilipatikana katika harambee hiyo ambayo mbunge wa kalenga Mh. Mgimwa amechangia milioni tano huku mwenyekiti wa CCM mkoa akisisitiza wote walioahidi kuwasilisha michango yao ndani ya wiki moja kupitia namba 0758804479


Mangula amekuwa mkuu wa wilaya kwa miaka sita, mkuu wa mkoa kwa mikoa tofauti kwa miaka saba, katibu mkuu wa CCM kwa miaka kumi na sasa makamu mwenyekiti wa CCM bara kwa miaka mitano hadi 2017 atakapokabidhi kijiti kwa wengine


MUNGU IBARIKI TUMAINI UNIVERSITY

MUNGU IBARIKI FAITH CHOIR
MUNGU IBARIKI CCT

Saturday, November 24, 2012


Kasoro katika mchakato utunzi mitihani, mitaala.

UTAFITI wa kitaalamu umeonyesha kuwapo kwa kasoro katika mchakato wa utunzi wa mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na kubainisha kuwa, kufeli kwa wanafunzi wa shule za sekondari kunatokana na walimu kutopewa mafunzo ya utekelezaji wa mitalaa.

Miongoni mwa kasoro zilizobainishwa ni pamoja na utata kuhusu nafasi za alama za mazoezi katika mtihani wa mwisho na ushiriki wa walimu na wakuzaji mitalaa katika utunzi wa mitihani hiyo.

Kadhalika matokeo ya utafiti huo ulioratibiwa na Shirika la HakiElimu, yanaitaja kasoro nyingine kuwa,ni baadhi ya mada za masomo kutungiwa maswali mengi, huku mada nyingine zikiachwa bila kutungiwa maswali kwa muda mrefu.

Hata hivyo, utafiti huo umeweka bayana kuwa, hakuna uhusiano wa moja kwa moja unaothibitisha kuwa mitihani inayotungwa ndio sababu ya wanafunzi kufeli, kwani kwa kiasi kikubwa maswali yanayotungwa yamekuwa yakiakisi kilichomo kwenye mitalaa
.
Akiwasilisha ripoti ya utafiti huo kwa wanahabari na wadau wa elimu jana, Mkuu wa Kitivo cha Elimu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE),  Dk Kitila Mkumbo alisema kuwa, tatizo lililopo ni walimu kutopatiwa mafunzo ya mitalaa, hasa inapofanyiwa uboreshaji na kuwapo kwa mazingira duni ya kufundishia na kujifunzia.

“Kuna ongezeko la wanafunzi kufeli mitihani yao ya mwisho na mara nyingi tumekuwa tukihusisha na sababu nyingine bila kuangalia ushiriki wa walimu katika uboreshaji wa mitaala,” alisema.
Alisema zaidi ya asilimia 80 ya walimu walioshiriki katika utafiti huo uliofanyika katika mikoa sita nchini, walisema Serikali haijawashirikisha katika uboreshaji wa mtalaa mpya unaotumika sasa, hivyo wanapata ugumu kuutekeleza. 

“Walimu wanabainisha kuwa , hawajashirikishwa katika mabadiliko ya mtalaa kutoka kwenye maudhui kwenda maarifa yanayomjengea ujuzi mwanafunzi hali inayosababisha wengi kufundisha kwa  mazoea,” alisema na kuongeza:

“Wengi wa wakuza mitaala na walimu, watekelezaji wa mtaala, mara chache hushirikishwa katika michakato ya utungaji na kwa ujumla hawaelewi michakato hii”.

Kuhusu mada kutotungiwa mtihani, Dk Mkumbo alitoa mfano wa somo la Baiolojia katika mtihani wa 2009, kwamba kati ya maswali 29, matano (asilimia 1&0 yalitoka kwenye mada moja tu ya usalama katika mazingira). Somo hilo lina mada 16.
Dk Mkumbo alisema japokuwa Serikali imekuwa ikitekeleza mtalaa unaomjengea mwanafunzi ujuzi tangu mwaka 2005, ni walimu wachache wanaoifahamu dhana na falsafa ya mtalaa huo.
Kuhusu alama za mazoezi Dk Mkumbo alisema hakuna makubaliano kati ya NECTA kwa upande mmoja, walimu na wakuza mitaala kwa upende mwingine, iwapo mazoezi yanajumuishwa katika mitihani ya mwisho awa watahiniwa.

Wakati maafisa wa NECTA wakidai kuwa mazoezi hujumuishwa katika matokeo ya mwisho ya watahiniwa, walimu na wakuza mitaala hawaamini kuwa kuna utaratibu huu,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utafiti, Habari na Machapisho wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Makoye Wangeleja alikiri kuwa, taasisi yake imekuwa ikiwashirikisha walimu kwa kiasi kidogo, hali aliyosema inatokana na kutokuwa na fedha za kutosha kwa ajili ya kazi hiyo.
“Ni kweli walimu hawajapewa mafunzo kutokana bajeti finyu, lakini tunapokea mapendekezo ya utafiti huu na kuahidi kuyafanyia kazi, lengo likiwa ni kuboresha kiwango cha elimu nchini,” alisema Wangeleja. 

Akizungumzia ushirikiano wa NECTA na taasisi nyingine alisema kuwa,  mahojiano yaliyofanywa yanaonyesha kuwa mchakato wa utungaji wa mitihani kwa kiwango kikubwa ni kazi ya maofisa wa NECTA, ijapokuwa wataalamu wa aina tofauti huombwa ushauri kwa kadri wanavyohitajika.

Mapendekezo,
Pamoja na mambo mengine, Dk Mkumbo alipendekeza kuwa, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na wadau wengine elimu waweka utaratibu endelevu wa kuwapatia walimu fursa za mafunzo ya kila mara kuhusu mtalaa mpya.

“Ni jambo muhimu kutafuta namna ya kuwaandaa walimu kujua dhana, falsafa na mahitaji ya mtalaa unaolenga maarifa ya ujuzi,” aliongeza.
Kadhalika alipendekeza uimarishwe ushirikiano na mawasiliano kati ya NECTA na Taasisi ya Elimu Tanzania, ili kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu mtaala unaomjengea mwanafunzi ujuzi kwa kuzingatia malengo na matokeo ya kujifunza yanavyopimwa.
Kwa karibu miaka mitano sasa, kiwango cha ufaulu katika mitihani ya Taifa hasa ya kidato cha nne, kimekuwa kikishuka, kiasi cha kusababisha mijadala mikubwa ya kitaifa.

Mathalani mwaka 2010 wanafunzi 177,021 sawa na asilimia 50 ya wanafunzi 354,042 waliofanya mtihani wa kidato cha nne walifeli kwa kupata daraja sifuri. Wanafunzi wengine 136,633, sawa na asilimia 38.6 walipata daraja la nne.

Utafiti wa HakiElimu ulifanyika katika mikoa sita ya Mwanza, Tabora, Kilimanjaro, Singida, Morogoro na Iringa ikihusisha walimu na wadau wengine wakiwamo wakuza mitaala na moafisa wa mitihani.

Na  Theophilo Felix
Chanzo ni gazeti la  mwananchi.

Friday, November 2, 2012


Mbunge amcharukia waziri Bungeni

  MBUNGE wa Tunduru Kusini, Mtutura Abdallah Mtutura (CCM) jana aliibana Serikali na kuitaka kuacha kutoa majibu ya uwongo ambayo yanapatikana kutoka kwa watuhumiwa.
Mtutura alitoa kauli hiyo baada ya kutokubaliana na majibu ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kuhusu kukanusha kuwa wananchi wa Tunduru hawateswi wala kupigwa wanapoingia kuvua samaki kandokando ya Mto Ruvuma.
“Mheshimiwa Spika, hivi itakuwaje kama nitaleta ushahidi hapa kuwa wananchi wanapigwa, wanateswa na kuporwa mali zao pindi wanapoingia katika maziwa na bahari kwa ajili ya kuvua samaki tu,” alihoji Mtutura na kuongeza.
“Maana ninachoona hapa ni kuwa Naibu Waziri amekuja na majibu ambayo kwa vyovyote ameyapata kutoka kwa watuhumiwa wa jambo hilo ndio maana anajibu hivyo majibu ambayo sikubaliani nayo.”
Katika swali la msingi Mbunge huyo alitaka kujua kwa nini wananchi wa Vijiji vya Wenje, Nasomba Makande, Kazamoyo, Misechele na Meyamtwaro vilivyo kandokando ya Mto Ruvuma wanasumbuliwa na askari wa maliasili kwa kupigwa na kunyang’anywa mali zao wanapovua samaki kama kitoweo.
Naibu Waziri alisema kuwa kutokana na wananchi wengi kuharibu mazingira kwenye maeneo ya wazi, kumesabisha upatikanaji mdogo wa samaki na hivyo hulazimika kuingia kwenye pori la Mwambesi kinyume na sheria na kuvua samaki huko.
Alisema wananchi hao wanapokutwa katika maeneo hayo, hukamatwa na kikosi cha doria na kupelekwa katika kituo cha Polisi kama taratibu za nchi zinavyoelekeza.
Hata hivyo alibainisha kuwa yapo matukio kadhaa ambayo hubainika kwa kisingizio cha kuvua samaki, lakini wananchi wanaingia na kufanya ujangili ndani ya hifadhi.
Waziri alilieleza kuwa Bunge kuwa hali ya ujangili hivi sasa ni kubwa nchini na majangili wengi huingia ndani ya hifadhi kwa lengo baya huku wakiwa na silaha nzito zikiwamo za kivita hivyo ni vema hata askari wa wanyamapori kuwa makini na jambo hilo.

Imewekwa na Moi Dodo
Chanzo ni gazeti la Mwananchi
 

Thursday, August 9, 2012


HATIMAYE MALAWI  WATII  KUFUNGASHA VILAGO ZIWA NYASA

 Na Theophilo Felix
siku chache baada ya Serikali kuzitaka ndege zinazozunguka Ziwa Nyasa upande wa Tanzania kufanya utafiti wa mafuta kuondoka mara moja, Serikali ya Malawi imetii na kuziondoa kampuni zinazofanya kazi hiyo katika ziwa hilo.

Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake Jumatatu iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliitaka Malawi kuziondoa ndege na kampuni zinazofanya utafiti wa mafuta katika eneo hilo kwa kuwa ni mali ya Tanzania.

Mbali na Waziri Membe, viongozi wengine waliozungumzia mgogoro huo na kuitaka Malawi iache uchokozi ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa.

Wakati Sitta akiwataka Watanzania kuendelea na shughuli zao bila hofu kwa kuwa Serikali iko tayari kwa tishio lolote, Lowassa alisisitiza kuwa Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo.

Jana kwa nyakati tofauti, Wakuu wa Wilaya nne zilizo mpakani mwa Tanzania na Malawi za Ileje, Mbozi, Mbeya, Kyela na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro walieleza kuwa mara baada ya kauli hizo, ndege hizo za Malawi ziliondoka na kampuni zilizokuwa zikitafiti mafuta katika Ziwa Nyasa zimeacha.
“Hapa tuko cool (tulivu) kabisa tangu zile ndege zilipoacha kuruka, tofauti na hizo kauli zinazotolewa na viongozi wa Serikali (ya Malawi),” alisema Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Dk Michael Kadeghe na kuongeza:

“Hapa niko kwenye Sherehe za Nanenane na Malawi wana banda lao nimetoka kulitembelea. Hali iko shwari, tunaendelea na uhusiano kama kawaida.”

Kuhusu mradi wa Bonde la Mto Songwe unaozihusisha Wilaya za Mbozi, Ileje, Rungwe, Mbeya Vijijini na Malawi, Dk Kadeghe alisema bado haujaathirika.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, Norman Sigalla alisema mgogoro huo kwa sasa uko kwenye hatua za awali hivyo ni vigumu kusema kuwa nchi inaweza kuingia vitani au la.
Kuhusu Mradi huo wa Bonde la Mto Songwe, Sigalla alisema bado haujaathirika kwa kuwa hakuna aliyekiuka makubaliano.

Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Rosemary Sengamule alisema: “Hapa kwetu tuko shwari kabisa, hata juzi nilikuwa na viongozi wa Malawi waliokuja hapa kwa ajili ya Mradi wa Bonde la Mto Songwe tukajadiliana jinsi ya kuuendeleza. Hata jana nimepita eneo la mpakani sijaona tishio lolote, labda huko Kyela.”

Kwa upande wake, Kandoro alisema: “Mimi naona tuko shwari, hakuna tishio lolote. Nadhani ulimsikia juzi Waziri wa Mambo ya Nje akisema. Tuache diplomasia ifanye kazi yake. Uhusiano wetu wa kidiplomasia na Malawi haujaharibika.”Kyela kazi kama kawaida

Wakazi wa Kyela wakiwamo wavuvi wanaofanya shughuli zao katika Ziwa Nyasa wamesema wanaendelea na kazi zao za kila siku kama kawaida licha ya kuibuka kwa mgogoro huo wa mpaka.

Wakizungumza na wandishi kwa nyakati tofauti, wananchi hao walisema licha ya kusikia mgogoro huo, bado wameendelea kuwa na uhusiano mzuri kati yao na Wamalawi.

Walisema kuwa tangu kuibuka kwa mjadala kuhusiana na mpaka huo wa Ziwa Nyasa, hakuna tatizo ambalo limeonekana miongoni mwao na kwamba muda wote wanaendelea na shughuli zao za mpakani.

Mkazi wa Kata ya Kabanga Songwe, Lusajo Mwakapisu alisema hakuna tukio lolote ambalo limeweza kuripotiwa kuhusiana na mgogoro unaoendelea baina ya nchi hizo mbili.

Alisema wanaendelea na shughuli zao kama kawaida na hakuna kizuizi chochote mpakani mwa Tanzania na Malawi na kwamba muda wote wamekuwa wakivuka mpaka na kuingia nchi hiyo jirani.

Wavuvi katika ziwa hilo walisema muda wote wapo kazini na hakuna kikwazo chochote kwao tangu kuripotiwa kwa mgogoro huo.

“Wenzetu wanadai ziwa lote lipo Malawi lakini, nyaraka zilizotengenezwa na wakoloni wa Kiingereza mwaka 1928 na 1938 zinaonyesha kuwa mpaka wa ziwa hilo upo katikati,” alisema.

Alisema hoja ya Tanzania ina nguvu kulingana na sheria za kimataifa kwa vile tatizo kama hilo linafanana na mgogoro uliokuwapo baina ya Cameroon na Nigeria. Alisema katika kesi iliyofunguliwa katika Mahakama Kuu ya Dunia, iliamuliwa kuwa mpaka baina ya nchi hizo mbili upite katikati ya Ziwa Chad ukifuata msitari ulionyooka.
 

Sunday, July 22, 2012

Haya ndio mapokezi ya Mabingwa wa Kopa Cocacola {2012} Morogoro




Tatizo la Maji litaisha lini?



Na. Hatibu jumbe
Ni miaka hamsini sasa tangu Tanzania ijipatie uhuru wake toka kwa wakolon,kwa lengo la kujiendeshea maisha yao wenyewe.Katika kipindi chote hicho bado suala la upatikanaji wa maji safi na salama limekuwa likisuasua hasa kwa wakazi wa vijijini.
Suala la upatikanaji wa maji limekuwa ni tatizo sugu la licha ya kuwepo kwa sera na kaulimbiu mbalimbali zinazo tolewa kila mwaka zikiwa na dhumuni la kuboresha na kurekebisha upatikanaji wa maji mijini na vijijini.

Si ajabu kuona misururu ya ndoo kwenye mabomba au watu na mikokoten yao kueleke bombani katika miji kadhaa hapo Tanzania. Imesha wahi kuriportiwa kupitia vyombo kadhaa vya habari kuwa mikioa ya Morogoro, Dodoma, Singida na baadhi ya maeneo ya Dar es sallam kukabiliwa na adha ya maji katika misimu mbalimbali ya majira.
Mara nyingi wahanga wakubwa wa janga hili ni wanawake ambao huwajibika kutafuta maji toka pale yanapopatikana mpaka nyumbani, ambapo maranyingi huyatoa umbali mrefu. Hali hii inakwamisha juhudi nzima ya maendeleo kwani badala ya watu kujumuika katika shughuli nyingine za kimaendeleo wanaishia kupanga misururu na foleni katika mabomba ya maji na vyanzo mbalimbali vya maji.

Maadhimisho ya wiki ya maji mwaka huu kitaifa yamefanyika mkoani Iringa yakiwa na kaulimbiu inayosema “Maji kwa Usalama wa Chakula” 

Mipango ya utekelezaji ya Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira iliyozinduliwa na rais Jakaya Kiwete mwaka 2007, ililenga kuongeza upatikanaji wa huduma za majisafi na salama katika miji mikuu 19 ya mikoa (ukiacha Dar es Salaam na Pwani) kutoka asilimia 78 mwaka 2006 hadi asilimia 90 mwezi Desemba mwaka 2010. Hadi ilipofika Desemba 2011, hali ya upatikanaji wa huduma za maji safi na salama katika miji hiyo ilikuwa asilimia 88 ambapo lengo halikufanikiwa kwa asilimia 2

Katika maeneo ya vijijini, lengo lilikuwa kuongeza Desemba mwaka 2006 hadi asilimia 65 ifikapo mwezi Desemba 2010. Hadi Desemba 2011, upatikanaji wa huduma za maji vijijini ulikuwa katika wastani wa asilimia 58, ikiashiria kuhitajika kwa juhudi za ziada ili tuweze kufikia lengo. Juhudi hizo za ziada ni pamoja na zile zinazohitajika kutekelezwa ili kuboresha huduma za maji katika Jiji la Dar es Salaam, katika miji mikuu ya wilaya na miji midogo.

Licha ya juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali na mashirika binafsi katika kutatua tatizo hili la maji ni kama mradi wa visima vijijini, dhahir kuwa juhudi hizo zimegonga mwamba kwani wananchi waliowengi wanakabiliwa na tatizo hili.
Hakuna asiye tambua kuwa ukosefu wa maji  huweza kuhatarisha maisha ya binadadamu na hata kupelekea kifo kwani maradhi mbalimbali ya milipuko huibuka kama kipindupindu kutokakana na kunywa maji yasiyo safi na salama.

Kwa namna moja ama nyingine wananchi wanahusika moja kwa moja katika kufaya rasilimali ya maji kupotea kwa kulima kando kando ya vyanzo vya maji au kukata miti.
Wote tumeshaona kile kinacho tokea Somalia jinsi watu na mifugo inavyoteketea kwa ukosefu wa maji.  Takwimu zinasema kwamba kutakuwa na ukosekanaji wa maji ifikapo mwaka 2025 endapo vyanzo vya maji vilivyopo sasa havitotunzwa.

Miradi mbalimbali imekuwa ikianzishwa kama vile za kilimo cha umwagiliaji, ufugaji huku sekta hizi zote zikiwa na vikwazo vikubwa vya ukosekanaji wa maji ya kutosha.
Hatunabudi wananchi tuunge mkono juhudi zinazofanywa na serikali juu ya upatikanaji wa maji safi na salama ikiwemo kutunza vyanzo vya maji na kuwafichua waharibifu wa vyanzo hivyo, pia tuache tabia ya kupasua mabomba ya maji.

Vilevile kwa upande wa serikali ihakikishe miradi anzilishwi ya maji ipewe watendaji waaminifu kwani baadhi ya watendaji kwenye kamati hizo hufanya ubadhirifu wa hela za miradi bila kujali wananchi wanaathirika kwa kiwango gani

Saturday, June 30, 2012

DOKTA ASHA-ROSE MIGIRO AWA MJUMBE WA MASUALA YA UKIMWI BARANI AFRIKA.


       Na Consolata Haule
         
      Aliyekuwa naibu katibu mkuu wa Umoja wa  Afrika dokta Asha-Rose Migiro         ameteuliwa    na katibu mkuu wa umoja wa mataifa   mheshimiwa Ban Ki Moon kuwa mjumbe wake maalum wa masuala ya Ukimwi barani afrika baada ya kumaliza mda wake.
    
       Alitangaza uteuzi huo katika hafla ya maaulum  aliyoondaa kwa ajili ya ya kumuuga Naibu Katibu Mkuu wake  ambaye amemaliza muda  wa uongozi  wake kwa muda wa miaka mitano na nusu katika nafasi ya  Unaibu Katibu  Mkuu.
  
        Hafla hiyo ilifanyika  katika wiwanja vya Umoja wa Mataifa na kuweza kuhudhuria na  wageni waalikwa wengi  mabalimbali na mashuhuru duniani wakiwemo mabalozi wan chi mbalimbali, wakuu wa mashirika  ya Umoja wa Mataifa. 
     
   Ametangaza rasmi kwamba amemteua dkt.  Asha- Rose Migiro kuwa  mjumbe wake maalum katika masuala ya ukimwi na ugonjwa wa Ukimwi Barani  Afrika. aliongeza kwa kusema  Ban Ki Moon. aliendelea kwa  kueleza kwamba ingawa Migiro alikuwa naibu katibu mkuu wake, lakini amekuwa mwalimu wake, na amejifunza mengi toka kwake na daima ataendelea kuuenzi mchango wake mkubwa aliofanya pindi alipokuwa kazini.

   “ Kama ni kuvaa viatu vyake, naweza kusema ningechekesha sana,  kwa ufupi siwezi kuvaa viatu vya Migiro, amekuwa msaada mkubwa sana kwangu, ameniwakilisha vema kila mahali nilipomtuma hata katika mazingira magumu na ya hatari,  kote ameniweza kuniwakalisha vema kiukweli. kama  mwalimu wangu, na kama profesa wangu anastahili alama ya juu sana” alisema  Ban Ki Moon na kushangiliwa.

   Alizidi kumuelezea  Migiro kama kiongozi si tu mwadilifu, lakini mwanadiplomasia  aliyebobea, aliyefanya kazi kubwa,ngumu na nzito kwa moyo mkunjufu, uhodari , umakini, na uadilifu wa hali ya juu sana.

    “ Siyo rahisi kuelezea yale aliyoyafanya nyuma ya pazia, namna gani alivyochapa kazi kwa nguvu, yapo mengi makubwa ambayo Migiro ameyafanya na  kuyakamilisha kwa uadilifu wa hali ya juu. Migiro ni mwanadiplomasia aliyebobea lakini ni mtu wa vitendo, vitendo ambavyo lazima utaona matunda yake” akabainisha Ban Ki Moon.

    Na kuongeza “  Migiro amefanya kazi na viongozi wagumu,  akiwemo aliyekuwa  Rais wa Libya Muammar  Quadaff aliyethubutu hata kumrushia katiba ya Umoja wa Mataifa, kiukweli ameweza kuzikuna nyonyo za watu wengi wakiwamo watu wanyonge na wenye matatizo mbalimbali duniani.Vilevile ameweza  kuondokana migogoro inayoendelea duniani. hivyo lakini Umoja wa  Mataifa hautasahau mchango wake.

      Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  alliweza kuitumia fursa hiyo  kwa kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini ya raisi wake Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kumruhusu Migiro kwenda kuitumikia jumuia ya kimataifa.

   “ Ninapenda  kutoa shukrani zangu za pekee kwa  jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa kumtoa Migiro katika utumishi wake wa Umma kuja kunisaidia , kwa serikali ya Tanzania na  watanzania nasema asanteni sana” alisema Ban Ki Moon..

     Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu dkt. Asha-Rose Migiro amesema anaupokea kwa mikono miwili uteuzi wa kuwa mjumbe maalum wa Katibu Mkuu katika masuala ya Ukimwi barani Afrika.

      Alizidi kusema   masuala ya  ukimwi na ugonjwa wa ukimwi, ni eneo ambalo limo ndani ya moyo wake na kwamba anashukuru kuona kwamba Katibu Mkuu anamuamini anaweza kumsaidia. Aliaahidi  atalitekeleza  jukumu  hilo kwa heshima  kubwa aliyopewa na Katibu Mkuu.
       Pia alimshukuru Ban Ki Moon kwa kumuamini kwamba anaweza kumsaidia kama naibu Katibu Mkuu, na akamshukuru pia kwa ushirikiano mkubwa na uhusiano mkubwa uliojengeka kati yake na Ban Ki Moon lakini pia kati yake na wasaidizi wake.  Ushirikiano ambao alisema ulichangia utendaji mzuri wa kazi na kufanikisha dira na matarajio ya Katibu Mkuu.

      “Katibu Mkuu amenipa heshima ya kihistoria, heshima ya kuwa msadizi wake,  ni heshima kubwa kwangu na kwa yeyote atakayekuja kuandika historia yangu, kwa namna yoyote ile hawezi kukwepa  kumtaja  Ban Ki Moon, naomba nikushukuru sana kwa heshima hii kubwa uliyonipa” alisema Migiro.

      Katika hafla hiyo pia ilihudhuriwa  na familia ya Naibu Katibu Mkuu ikijumuisha  mume wake, Profesa  Cleophas Migiro,  mdogo wa  Naibu Katibu Mkuu, Bi. Amina  Mtengeti na mtoto wao wa  mwisho wa Migiro Chansa Jasmin.

    Naibu Katibu Migiro anakuwa mwanamke wa pili kushika wadhifa huo na mwanamke mwafrika wa kwanza. Lakini pia ni naibu katibu mkuu ambaye amehudumu katika wadhifa huo kwa miaka mitano na nusu.
Dokta Asha-Rose Migiro akizungumza na kutoa shukrani katika hafla hiyo.

         Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa anazungumza na wageni waalikwa hawapo pichani,kulia  ni Dkt. Migiro na katikati ni Mkurugenzi wa ofisi ya Naibu Katibu Mkuu, Bwana  Anyanga