Na
Consolata Haule
Aliyekuwa naibu
katibu mkuu wa Umoja wa Afrika dokta
Asha-Rose Migiro ameteuliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa mheshimiwa Ban Ki Moon kuwa mjumbe wake
maalum wa masuala ya Ukimwi barani afrika baada ya kumaliza mda wake.
Alitangaza uteuzi
huo katika hafla ya maaulum aliyoondaa
kwa ajili ya ya kumuuga Naibu Katibu Mkuu wake
ambaye amemaliza muda wa
uongozi wake kwa muda wa miaka mitano na
nusu katika nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu.
Hafla hiyo
ilifanyika katika wiwanja vya Umoja wa
Mataifa na kuweza kuhudhuria na wageni
waalikwa wengi mabalimbali na mashuhuru
duniani wakiwemo mabalozi wan chi mbalimbali, wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Ametangaza rasmi kwamba amemteua dkt.
Asha- Rose Migiro kuwa mjumbe wake maalum katika masuala ya ukimwi na
ugonjwa wa Ukimwi Barani Afrika. aliongeza kwa kusema Ban Ki Moon.
aliendelea kwa kueleza kwamba ingawa Migiro alikuwa naibu katibu mkuu
wake, lakini amekuwa mwalimu wake, na amejifunza mengi toka kwake na daima
ataendelea kuuenzi mchango wake mkubwa aliofanya pindi alipokuwa kazini.
“ Kama ni kuvaa viatu vyake, naweza kusema
ningechekesha sana, kwa ufupi siwezi kuvaa
viatu vya Migiro, amekuwa msaada mkubwa sana
kwangu, ameniwakilisha vema kila mahali nilipomtuma hata katika mazingira
magumu na ya hatari, kote ameniweza kuniwakalisha vema kiukweli.
kama mwalimu wangu, na kama profesa wangu anastahili alama ya juu sana” alisema Ban Ki
Moon na kushangiliwa.
Alizidi kumuelezea Migiro kama
kiongozi si tu mwadilifu, lakini mwanadiplomasia aliyebobea, aliyefanya
kazi kubwa,ngumu na nzito kwa moyo mkunjufu, uhodari , umakini, na uadilifu wa
hali ya juu sana.
“ Siyo rahisi kuelezea yale aliyoyafanya
nyuma ya pazia, namna gani alivyochapa kazi kwa nguvu, yapo mengi makubwa
ambayo Migiro ameyafanya na kuyakamilisha kwa uadilifu wa hali ya juu.
Migiro ni mwanadiplomasia aliyebobea lakini ni mtu wa vitendo, vitendo ambavyo
lazima utaona matunda yake” akabainisha Ban Ki Moon.
Na kuongeza “ Migiro amefanya kazi na
viongozi wagumu, akiwemo aliyekuwa Rais wa Libya Muammar
Quadaff aliyethubutu hata kumrushia katiba ya Umoja wa Mataifa, kiukweli
ameweza kuzikuna nyonyo za watu wengi wakiwamo watu wanyonge na wenye matatizo
mbalimbali duniani.Vilevile ameweza kuondokana migogoro inayoendelea
duniani. hivyo lakini Umoja wa Mataifa hautasahau mchango wake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,
alliweza kuitumia fursa hiyo kwa kuishukuru serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania
nchini ya raisi wake Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kumruhusu Migiro
kwenda kuitumikia jumuia ya kimataifa.
“ Ninapenda kutoa shukrani zangu za
pekee kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa kumtoa Migiro katika
utumishi wake wa Umma kuja kunisaidia , kwa serikali ya Tanzania na
watanzania nasema asanteni sana” alisema Ban Ki Moon..
Kwa upande wake,
Naibu Katibu Mkuu dkt. Asha-Rose Migiro amesema anaupokea kwa mikono miwili
uteuzi wa kuwa mjumbe maalum wa Katibu Mkuu katika masuala ya Ukimwi barani
Afrika.
Alizidi kusema masuala
ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi, ni eneo ambalo limo ndani ya moyo wake na
kwamba anashukuru kuona kwamba Katibu Mkuu anamuamini anaweza kumsaidia. Aliaahidi
atalitekeleza jukumu hilo
kwa heshima kubwa aliyopewa na Katibu Mkuu.
Pia alimshukuru Ban Ki Moon
kwa kumuamini kwamba anaweza kumsaidia kama
naibu Katibu Mkuu, na akamshukuru pia kwa ushirikiano mkubwa na uhusiano mkubwa
uliojengeka kati yake na Ban Ki Moon lakini pia kati yake na wasaidizi
wake. Ushirikiano ambao alisema ulichangia utendaji mzuri wa kazi na
kufanikisha dira na matarajio ya Katibu Mkuu.
“Katibu Mkuu amenipa heshima ya
kihistoria, heshima ya kuwa msadizi wake, ni heshima kubwa kwangu na kwa
yeyote atakayekuja kuandika historia yangu, kwa namna yoyote ile hawezi
kukwepa kumtaja Ban Ki Moon, naomba nikushukuru sana kwa heshima
hii kubwa uliyonipa” alisema Migiro.
Katika hafla hiyo pia ilihudhuriwa
na familia ya Naibu Katibu Mkuu ikijumuisha mume wake, Profesa
Cleophas Migiro, mdogo wa Naibu Katibu Mkuu, Bi. Amina
Mtengeti na mtoto wao wa mwisho wa Migiro Chansa Jasmin.
Naibu Katibu Migiro anakuwa mwanamke wa
pili kushika wadhifa huo na mwanamke mwafrika wa kwanza. Lakini pia ni naibu
katibu mkuu ambaye amehudumu katika wadhifa huo kwa miaka mitano na nusu.
Dokta Asha-Rose Migiro akizungumza na kutoa shukrani katika hafla hiyo.