Sunday, July 22, 2012

Haya ndio mapokezi ya Mabingwa wa Kopa Cocacola {2012} Morogoro




Tatizo la Maji litaisha lini?



Na. Hatibu jumbe
Ni miaka hamsini sasa tangu Tanzania ijipatie uhuru wake toka kwa wakolon,kwa lengo la kujiendeshea maisha yao wenyewe.Katika kipindi chote hicho bado suala la upatikanaji wa maji safi na salama limekuwa likisuasua hasa kwa wakazi wa vijijini.
Suala la upatikanaji wa maji limekuwa ni tatizo sugu la licha ya kuwepo kwa sera na kaulimbiu mbalimbali zinazo tolewa kila mwaka zikiwa na dhumuni la kuboresha na kurekebisha upatikanaji wa maji mijini na vijijini.

Si ajabu kuona misururu ya ndoo kwenye mabomba au watu na mikokoten yao kueleke bombani katika miji kadhaa hapo Tanzania. Imesha wahi kuriportiwa kupitia vyombo kadhaa vya habari kuwa mikioa ya Morogoro, Dodoma, Singida na baadhi ya maeneo ya Dar es sallam kukabiliwa na adha ya maji katika misimu mbalimbali ya majira.
Mara nyingi wahanga wakubwa wa janga hili ni wanawake ambao huwajibika kutafuta maji toka pale yanapopatikana mpaka nyumbani, ambapo maranyingi huyatoa umbali mrefu. Hali hii inakwamisha juhudi nzima ya maendeleo kwani badala ya watu kujumuika katika shughuli nyingine za kimaendeleo wanaishia kupanga misururu na foleni katika mabomba ya maji na vyanzo mbalimbali vya maji.

Maadhimisho ya wiki ya maji mwaka huu kitaifa yamefanyika mkoani Iringa yakiwa na kaulimbiu inayosema “Maji kwa Usalama wa Chakula” 

Mipango ya utekelezaji ya Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira iliyozinduliwa na rais Jakaya Kiwete mwaka 2007, ililenga kuongeza upatikanaji wa huduma za majisafi na salama katika miji mikuu 19 ya mikoa (ukiacha Dar es Salaam na Pwani) kutoka asilimia 78 mwaka 2006 hadi asilimia 90 mwezi Desemba mwaka 2010. Hadi ilipofika Desemba 2011, hali ya upatikanaji wa huduma za maji safi na salama katika miji hiyo ilikuwa asilimia 88 ambapo lengo halikufanikiwa kwa asilimia 2

Katika maeneo ya vijijini, lengo lilikuwa kuongeza Desemba mwaka 2006 hadi asilimia 65 ifikapo mwezi Desemba 2010. Hadi Desemba 2011, upatikanaji wa huduma za maji vijijini ulikuwa katika wastani wa asilimia 58, ikiashiria kuhitajika kwa juhudi za ziada ili tuweze kufikia lengo. Juhudi hizo za ziada ni pamoja na zile zinazohitajika kutekelezwa ili kuboresha huduma za maji katika Jiji la Dar es Salaam, katika miji mikuu ya wilaya na miji midogo.

Licha ya juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali na mashirika binafsi katika kutatua tatizo hili la maji ni kama mradi wa visima vijijini, dhahir kuwa juhudi hizo zimegonga mwamba kwani wananchi waliowengi wanakabiliwa na tatizo hili.
Hakuna asiye tambua kuwa ukosefu wa maji  huweza kuhatarisha maisha ya binadadamu na hata kupelekea kifo kwani maradhi mbalimbali ya milipuko huibuka kama kipindupindu kutokakana na kunywa maji yasiyo safi na salama.

Kwa namna moja ama nyingine wananchi wanahusika moja kwa moja katika kufaya rasilimali ya maji kupotea kwa kulima kando kando ya vyanzo vya maji au kukata miti.
Wote tumeshaona kile kinacho tokea Somalia jinsi watu na mifugo inavyoteketea kwa ukosefu wa maji.  Takwimu zinasema kwamba kutakuwa na ukosekanaji wa maji ifikapo mwaka 2025 endapo vyanzo vya maji vilivyopo sasa havitotunzwa.

Miradi mbalimbali imekuwa ikianzishwa kama vile za kilimo cha umwagiliaji, ufugaji huku sekta hizi zote zikiwa na vikwazo vikubwa vya ukosekanaji wa maji ya kutosha.
Hatunabudi wananchi tuunge mkono juhudi zinazofanywa na serikali juu ya upatikanaji wa maji safi na salama ikiwemo kutunza vyanzo vya maji na kuwafichua waharibifu wa vyanzo hivyo, pia tuache tabia ya kupasua mabomba ya maji.

Vilevile kwa upande wa serikali ihakikishe miradi anzilishwi ya maji ipewe watendaji waaminifu kwani baadhi ya watendaji kwenye kamati hizo hufanya ubadhirifu wa hela za miradi bila kujali wananchi wanaathirika kwa kiwango gani