Sunday, July 22, 2012
Tatizo la Maji litaisha lini?
Na. Hatibu jumbe
Ni miaka
hamsini sasa tangu Tanzania ijipatie uhuru wake toka kwa wakolon,kwa lengo la
kujiendeshea maisha yao wenyewe.Katika kipindi chote hicho bado suala la
upatikanaji wa maji safi na salama limekuwa likisuasua hasa kwa wakazi wa
vijijini.
Suala la
upatikanaji wa maji limekuwa ni tatizo sugu la licha ya kuwepo kwa sera na
kaulimbiu mbalimbali zinazo tolewa kila mwaka zikiwa na dhumuni la kuboresha na
kurekebisha upatikanaji wa maji mijini na vijijini.
Si ajabu
kuona misururu ya ndoo kwenye mabomba au watu na mikokoten yao
kueleke bombani katika miji kadhaa hapo Tanzania. Imesha wahi kuriportiwa
kupitia vyombo kadhaa vya habari kuwa mikioa ya Morogoro, Dodoma, Singida na baadhi ya maeneo ya Dar es
sallam kukabiliwa na adha ya maji katika misimu mbalimbali ya majira.
Mara nyingi
wahanga wakubwa wa janga hili ni wanawake ambao huwajibika kutafuta maji toka
pale yanapopatikana mpaka nyumbani, ambapo maranyingi huyatoa umbali mrefu.
Hali hii inakwamisha juhudi nzima ya maendeleo kwani badala ya watu kujumuika
katika shughuli nyingine za kimaendeleo wanaishia kupanga misururu na foleni
katika mabomba ya maji na vyanzo mbalimbali vya maji.
Maadhimisho
ya wiki ya maji mwaka huu kitaifa yamefanyika mkoani Iringa yakiwa na kaulimbiu
inayosema “Maji kwa Usalama wa Chakula”
Mipango ya
utekelezaji ya Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira iliyozinduliwa na rais
Jakaya Kiwete mwaka 2007, ililenga kuongeza upatikanaji wa huduma za majisafi
na salama katika miji mikuu 19 ya mikoa (ukiacha Dar es Salaam na Pwani) kutoka
asilimia 78 mwaka 2006 hadi asilimia 90 mwezi Desemba mwaka 2010. Hadi
ilipofika Desemba 2011, hali ya upatikanaji wa huduma za maji safi na salama
katika miji hiyo ilikuwa asilimia 88 ambapo lengo halikufanikiwa kwa asilimia 2
Katika
maeneo ya vijijini, lengo lilikuwa kuongeza Desemba mwaka 2006 hadi asilimia 65
ifikapo mwezi Desemba 2010. Hadi Desemba 2011, upatikanaji wa huduma za maji
vijijini ulikuwa katika wastani wa asilimia 58, ikiashiria kuhitajika kwa
juhudi za ziada ili tuweze kufikia lengo. Juhudi hizo za ziada ni pamoja na zile
zinazohitajika kutekelezwa ili kuboresha huduma za maji katika Jiji la Dar es
Salaam, katika miji mikuu ya wilaya na miji midogo.
Licha ya
juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali na mashirika binafsi katika kutatua
tatizo hili la maji ni kama mradi wa visima vijijini, dhahir kuwa juhudi hizo
zimegonga mwamba kwani wananchi waliowengi wanakabiliwa na tatizo hili.
Hakuna asiye
tambua kuwa ukosefu wa maji huweza
kuhatarisha maisha ya binadadamu na hata kupelekea kifo kwani maradhi
mbalimbali ya milipuko huibuka kama kipindupindu kutokakana na kunywa maji
yasiyo safi na salama.
Kwa namna
moja ama nyingine wananchi wanahusika moja kwa moja katika kufaya rasilimali ya
maji kupotea kwa kulima kando kando ya vyanzo vya maji au kukata miti.
Wote
tumeshaona kile kinacho tokea Somalia jinsi watu na mifugo inavyoteketea kwa
ukosefu wa maji. Takwimu zinasema kwamba
kutakuwa na ukosekanaji wa maji ifikapo mwaka 2025 endapo vyanzo vya maji
vilivyopo sasa havitotunzwa.
Miradi
mbalimbali imekuwa ikianzishwa kama vile za kilimo cha umwagiliaji, ufugaji
huku sekta hizi zote zikiwa na vikwazo vikubwa vya ukosekanaji wa maji ya
kutosha.
Hatunabudi
wananchi tuunge mkono juhudi zinazofanywa na serikali juu ya upatikanaji wa
maji safi na salama ikiwemo kutunza vyanzo vya maji na kuwafichua waharibifu wa
vyanzo hivyo, pia tuache tabia ya kupasua mabomba ya maji.
Saturday, June 30, 2012
DOKTA ASHA-ROSE MIGIRO AWA MJUMBE WA MASUALA YA UKIMWI BARANI AFRIKA.
Na
Consolata Haule
Aliyekuwa naibu
katibu mkuu wa Umoja wa Afrika dokta
Asha-Rose Migiro ameteuliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa mheshimiwa Ban Ki Moon kuwa mjumbe wake
maalum wa masuala ya Ukimwi barani afrika baada ya kumaliza mda wake.
Alitangaza uteuzi
huo katika hafla ya maaulum aliyoondaa
kwa ajili ya ya kumuuga Naibu Katibu Mkuu wake
ambaye amemaliza muda wa
uongozi wake kwa muda wa miaka mitano na
nusu katika nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu.
Hafla hiyo
ilifanyika katika wiwanja vya Umoja wa
Mataifa na kuweza kuhudhuria na wageni
waalikwa wengi mabalimbali na mashuhuru
duniani wakiwemo mabalozi wan chi mbalimbali, wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Ametangaza rasmi kwamba amemteua dkt.
Asha- Rose Migiro kuwa mjumbe wake maalum katika masuala ya ukimwi na
ugonjwa wa Ukimwi Barani Afrika. aliongeza kwa kusema Ban Ki Moon.
aliendelea kwa kueleza kwamba ingawa Migiro alikuwa naibu katibu mkuu
wake, lakini amekuwa mwalimu wake, na amejifunza mengi toka kwake na daima
ataendelea kuuenzi mchango wake mkubwa aliofanya pindi alipokuwa kazini.
“ Kama ni kuvaa viatu vyake, naweza kusema
ningechekesha sana, kwa ufupi siwezi kuvaa
viatu vya Migiro, amekuwa msaada mkubwa sana
kwangu, ameniwakilisha vema kila mahali nilipomtuma hata katika mazingira
magumu na ya hatari, kote ameniweza kuniwakalisha vema kiukweli.
kama mwalimu wangu, na kama profesa wangu anastahili alama ya juu sana” alisema Ban Ki
Moon na kushangiliwa.
Alizidi kumuelezea Migiro kama
kiongozi si tu mwadilifu, lakini mwanadiplomasia aliyebobea, aliyefanya
kazi kubwa,ngumu na nzito kwa moyo mkunjufu, uhodari , umakini, na uadilifu wa
hali ya juu sana.
“ Siyo rahisi kuelezea yale aliyoyafanya
nyuma ya pazia, namna gani alivyochapa kazi kwa nguvu, yapo mengi makubwa
ambayo Migiro ameyafanya na kuyakamilisha kwa uadilifu wa hali ya juu.
Migiro ni mwanadiplomasia aliyebobea lakini ni mtu wa vitendo, vitendo ambavyo
lazima utaona matunda yake” akabainisha Ban Ki Moon.
Na kuongeza “ Migiro amefanya kazi na
viongozi wagumu, akiwemo aliyekuwa Rais wa Libya Muammar
Quadaff aliyethubutu hata kumrushia katiba ya Umoja wa Mataifa, kiukweli
ameweza kuzikuna nyonyo za watu wengi wakiwamo watu wanyonge na wenye matatizo
mbalimbali duniani.Vilevile ameweza kuondokana migogoro inayoendelea
duniani. hivyo lakini Umoja wa Mataifa hautasahau mchango wake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,
alliweza kuitumia fursa hiyo kwa kuishukuru serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania
nchini ya raisi wake Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kumruhusu Migiro
kwenda kuitumikia jumuia ya kimataifa.
“ Ninapenda kutoa shukrani zangu za
pekee kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa kumtoa Migiro katika
utumishi wake wa Umma kuja kunisaidia , kwa serikali ya Tanzania na
watanzania nasema asanteni sana” alisema Ban Ki Moon..
Kwa upande wake,
Naibu Katibu Mkuu dkt. Asha-Rose Migiro amesema anaupokea kwa mikono miwili
uteuzi wa kuwa mjumbe maalum wa Katibu Mkuu katika masuala ya Ukimwi barani
Afrika.
Alizidi kusema masuala
ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi, ni eneo ambalo limo ndani ya moyo wake na
kwamba anashukuru kuona kwamba Katibu Mkuu anamuamini anaweza kumsaidia. Aliaahidi
atalitekeleza jukumu hilo
kwa heshima kubwa aliyopewa na Katibu Mkuu.
Pia alimshukuru Ban Ki Moon
kwa kumuamini kwamba anaweza kumsaidia kama
naibu Katibu Mkuu, na akamshukuru pia kwa ushirikiano mkubwa na uhusiano mkubwa
uliojengeka kati yake na Ban Ki Moon lakini pia kati yake na wasaidizi
wake. Ushirikiano ambao alisema ulichangia utendaji mzuri wa kazi na
kufanikisha dira na matarajio ya Katibu Mkuu.
“Katibu Mkuu amenipa heshima ya
kihistoria, heshima ya kuwa msadizi wake, ni heshima kubwa kwangu na kwa
yeyote atakayekuja kuandika historia yangu, kwa namna yoyote ile hawezi
kukwepa kumtaja Ban Ki Moon, naomba nikushukuru sana kwa heshima
hii kubwa uliyonipa” alisema Migiro.
Katika hafla hiyo pia ilihudhuriwa
na familia ya Naibu Katibu Mkuu ikijumuisha mume wake, Profesa
Cleophas Migiro, mdogo wa Naibu Katibu Mkuu, Bi. Amina
Mtengeti na mtoto wao wa mwisho wa Migiro Chansa Jasmin.
Naibu Katibu Migiro anakuwa mwanamke wa
pili kushika wadhifa huo na mwanamke mwafrika wa kwanza. Lakini pia ni naibu
katibu mkuu ambaye amehudumu katika wadhifa huo kwa miaka mitano na nusu.
Dokta Asha-Rose Migiro akizungumza na kutoa shukrani katika hafla hiyo.
Thursday, June 28, 2012
COCA COLA WAANDAA TUZO ZA WAANDISHI BORA WA MICHEZO WA COPA COCA COLA
Na Consolata haule
Coca-Cola Tanzania imetangaza kuanzisha tuzo kwa waandishi bora wa
michuano ya soka ya vijana ya Copa Coca-Cola kwa nia ya kuwazawadia
wanahabari wanaofanya kazi nzuri katika michezo,hivyo kuwa chachu ya mashindano ya Copa-Cola
yenye lengo la kujenga
msingi wa maendeleo ya soka nchini Tanzania.
Akizungumza na wandishi wa
habari jijini Dar es Salaam Meneja Masoko wa Coca Tanzania Salome Mabirizi
alisema kuwa Coca-cola inatambua mchango mkubwa uliofanywa na waadishi wa habari
kwa miaka mitano iliyopita katika kuwahamasisha kushiriki mashindano haya. Kuanzishwa kwa tuzo hizi ni njia moja wapo ya
kuwashukuru waandishi wa habari kwa kazi nzuri ya kutangaza Coca-Cola.
Alizitaja tuzo
hizo kuwa ni mwandishi bora wa magazeti, mwandishi bora wa luninga, mwanahabari
bora wa radio, mpiga picha bora (magazeti) na blogs bora, ambapo kila mshindi
ataweza kuzawadiwa thamani ya milioni 2 taslimu za kitanzania.
Mchakato wa kuwapata
washindi utafanywa kwa kushirikiana na Chama cha waandishi wa Habari za Michezo
Tanzania (TASWA) na Coca-Cola na tayari zoezi hilo limeshaanza tangu Jumapili
juni 24 wakati fainali za Copa Coca-Cola Taifa zilipozinduliwa rasmi jijini Dar
es Salaam na Fainali hizo zimepangwa kumalizika Julai 15.
Katibu Mkuu Msaidizi wa
TASWA, George John aliwaambia waandishi wa habari kuwa kamati ya tuzo za Copa
Coca-Cola itafanya kazi kwa kuzingatia vigezo ili kuweza kumpata mshindi anayestahili
katika kila kundi lililotaja hapo juu.Pia amevitaja baadhi ya
vigezo hivyo kuwa ni pamoja na stori au makala zinazohamasisha na kuwatia moyo
vijana kuweza kuonyesha na kuendeleza vipaji vyao.
Johan ameipongeza kampuni
ya Coca-Cola kwa kushirikiana na Shirika la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
kuendesha mashindano hyo kwa nchi nzima kwa lengo la kuibua vipaji vya wanasoka
chipukizi nchini Tanzania.
Kiukweli Copa Caca_Cola imesaidia
kubadili sura ya mpira wa miguu nchini Tanzania kwa kuwa chanzo cha kutegemewana wachezaji wenye vipaji wa kila timu za ligi kuu na timu za Taifa.
NI mashindano pekee nchini ambayo huchezwa nchi
nzima kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa yakishirikisha maelefu ya vijana kila
mwaka ili kuwaendeleza vijana
zaidi.
Coca-Cola imekuwa ikipeleka
wachezaji bora wa Copa Coca-Cola kwenye kambi za kimataifa za mafunzo ya soka
nchi za nje. Mnamo Mwaka 2007 na 2008
wachezaji bora wa Copa Coca-Cola walikwenda nchini Brazil na kuanzia 2008 hadi
mwaka jana walipelekwa Afrika Kusini.
Coca-Cola ni kampuni yenye
historia ndefu ya kusaidia michezo ilianza kudhamini michezo ya olimpiki tangu
1928 na mpira wa miguu tangu 1930.
Kampuni ya Coca-Cola imekuwa ikidhamini Shirikisho la mpira wa miguu
duniani (FIFA) tangu 1974 na kuwa mdhamini rasmi wa FIFA tangu 1978 hadi sasa.
Mkurugenzi mahusiano wa Coca Cola Kwanza( wa katikati )Bw. Evans Mlelwa
akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za Coca Cola juu ya Tuzo kwa waandishi wa habari COPA COCA
COLA,wa kwanza kulia ni Katibu msaidizi wa Taswa Bw. George John,kwa upande wa kushoto ni Meneja Masoko wa Coca Cola Tanzania Bi.Salome Mabirizi.
HALI YA DK. ULIMBOKA ILIVYO SASA.
Kama tunavyomwona Dk Ulimboka akiwa katika hali mbaya na huku akiwa ametundikiwa mashine maalum katika chumba cha wagonjwa wa mahututi katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili- Dar- es -salaam.
Na Consolata Haule
MADAKTARI WAPATAO 72 WASIMAMISHWA KAZI MKOANI MBEYA.
Na Consolata Haule
Bodi
ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, imewafukuza madaktari wapatao
72 kwa kosa la kutoingia kazini kwa siku tano jambo ambalo ni kinyume
cha makubaliano ya mkataba wao wa kazini.
Inasemekana kuwa madaktari hao ambao 54 ni wale wa mafunzo ambao waliingia mkataba
wa miaka miwili na hospitali ya Rufaa na madaktari 18 ni wale
walioajiriwa na Wizara ya afya.
Mwenyekiti wa Bodi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Norman Sigara, alisema kitendo cha madaktari kutoripoti kazini kwa siku
tano ni ukiukwaji wa kanuni za utumisha wa umma hivyo
kupitia kanuni hiyo ya utumishi wa umma madaktari hao wamesimamishwa kazi na kurudishwa kwa
mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa
hatua zaidi za kinidhamu alizidi kunena.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti huyo wa Bodi, imeelezwa kuwa siku ya tarehe
23/6/2012 wafanyakazi 15 waliokuwa zamu hawakufika kazini na tarehe 24/6/2012 wafanyakazi 19 hawakufika kazini.
Alizidi kusema kuwa kuanzia tarehe 25/6/2012 hadi leo imethibitika kuwa 72 hawakufika kazini hadi leo tarehe 28/6/2012.Na mnamo tarehe 25/6/2012 bodi ya hospitali ilifanya kikao cha dharura ili kujadili
hali ya utendaji kazi na utoaji huduma hospitalini na kutoa uamuzi juu ya jambo ilo.
Aliyataja maamuzi hayo kuwa ni Mwenyekiti wa Bodi akutane na madaktari
ambao hawakufika kazini ili awasikilize sababu za kutofika na kujadili
namna ya kumaliza matatizo hayo jambo ambalo madaktari hao waligoma.
Baada ya madaktari hao kukaidi ombi hilo, Bodi ya hospitali iliwaandikia barua za kujieleza kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu
kwa kuvunja mkataba walioingia na hospitali na pia kukiuka kanuni za
kudumu za utumishi wa umma nalo walilikaidi
Alizidi kuongeza kwamba iwapo
madaktari ambao hawakuripoti au kueleza sababu za kuridhisha ifikapo mpaka
tarehe 28/6/2012na kwa kuzingatia kanuni za utumishi wa Umma, madaktari
hao watasimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu
Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Vilevile alisema kuwa kwa ujumla madaktari hao waligomea barua zote mbili yaani
ya kuitwa kwenye kikao pamoja na ile ya kuwataka kujieleza hivyo Bodi
imechukua hatua za kisheria za kuwafukuza kazi.
Hata
hivyo Mwenyekiti huyo wa bodi, alisema kuwa tayari hospitali ya Rufaa
kwa ushirikiano wa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, madaktari watano
wamepatikana ili kusaidia huduma kwa hospitali hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Norman Sigara akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu kufukuzwa kazi kwa madaktari hao wapatao 72.
Subscribe to:
Posts (Atom)




