Saturday, January 21, 2012

BAJ WATANDAZA KANDANDA SAFI DHIDI YA MAENDELEO YA JAMII

Na Solomon Lekui
Full beki ya timu ya BAJ1 OLE LEKUI

Katika kuonesha kwamba timu ya wanafunzi wa Bachelor of Arts in Journalism kimejizatiti vizuri katika mpira wa miguu ( football) jana timu ya mwaka wa kwanza ilionesha kandanda la kitabuni baada ya kucheza pasi nyingi na safi zilizoifanya timu ya wapinzani wao BACD kuomba mechi kumalizika kabla ya wakati baada ya kuchoshwa na kandanda safi liloneshwa na vijana wa BAJ1. Mchezo huo ulianza kurindima kwenye mishale ya saa 11 na kumalizika saa moja kasoro.

Pamoja na kuonesha kandanda safi timu hizo zilitoka suluhu ya kufungana magoli 2-2 lakini mchezaji mmoja wa BACD aliumia vibaya sehemu za mbavu tukio lililopelekea kulazwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi.
Mashabiki nao hawajaachwa nyuma kwa kushangilia na kutia moyo huku wakiimba nyimbo za uhamasishaji kama vile "usiniumizieeeee....." watu weweeeeee                                      



wachezaji wa BAJ oscar,zephania pamoja na goalkeeper on duty waisaka chacha a.k.a "MURA"
Hawa ndio baadhi ya wachezaji wa timu ya BAJ kutoka kulia ni Oscar a.k.a mzee wa kiatu, katikati ni hija mkali a.k.a panya buku na ole lekui a.ka. beki mstaarabu

Hii ni baada ya mechi wachezaji wakajiunga na mashabiki wao kucheza kiduku

No comments:

Post a Comment