Friday, January 20, 2012

HATUKO NAE TENA ALIYEKUWA NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MBUNGE WA ARUMERU MH; JEREMIAH SUMARI

   Ni masikito na huzuni kubwa kwa wananchi wa Tanzania kupoteza mmoja wa watu mashuhuri Tanzania ambaye alikuwa mbunge wa Arumeru Mashariki kupitia chama tawala (CCM) na naibu waziri wa Fedha wa awamu ya nne kupitia uongozi wa Mh. Rais JAKAYA MRISHO KIKWETE.              
                 Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa SARATANI YA UBONGO kwa muda mrefu  sana na mnamo mwaka 2010 aliweza kumpelekwa nchini INDIA kwa matibabu zaidi ya upasuajina aliweza kupata nafuu.Mwishoni wa mwaka 2011 hali yake ilianza kuwa tete tena na tarehe 9,January,2012 alilazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili  ambapo siku ya alhamisi ya tarehe 19,January,2012 alitutoka duniani.



                                                      MAREHEMU JEREMIAH SUMARI.



                   Hivyo kutokana na msiba huo kamati ya bunge kushirikiana na familia na chama chake (CCM) wameandaa shughuli nzima ya kuuaga rasmi mwili wa marehemu siku ya Jumamosi tarehe 21,January katika viwanja vya KARIMJEE kuanzia mida ya saa 5 asubuhi  na siku ya jumapili kuweza kusafirisha kuelekea kijijini kwao     AKERI,MERU,mkoani ARUSHA kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika siku ya Jumatatu ya tar 22,january.2012.

                     Marehemu ameacha mjane na watoto wanne(4).     
                    
                               MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU 
                                              MAHALI PEMA PEPONI.
                                                         AMINA.
       "BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA  LIBARIKIWE"
                                                                                                                       Na Consolata Haule

No comments:

Post a Comment