Thursday, November 10, 2011

Serikali haijatoa suluhisho la kudumu migomo elimu ya juu.






Na John Alex.

Malalamiko yanayoendelea kutolewa na wanafunzi wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini ni dalili sio tu ya   wasomi hao kutokuridhishwa na hatua  zinazochukuliwa na serikali  katika kutatua changamoto  zinazowakabili  lakini pia  kushindwa vikali kwa serikali  iliyoko madarakani katika utekelezaji wa sera  zake kuhusu elimu  ya juu nchini.

Wote mtakubaliana na mimi kuwa wasomi wa vyuo vikuu nchini ni hazina kubwa sana kwa taifa la Tanzania  kwani hao ndio chimbuko la mawazo mapya na uelewa na  pia ni chazo  kikubwa sana cha maendeleo ya taifa. letu kwani  taifa bila wasomi ni sawa na  Gari  kubwa la mkaa litembealo njiani usiku bila  taa wakati wowote laweza gonga mti  au mwamba na kupinduka..

Matatizo yanayowakabili wanafunzi wasomi wa vyuo vikuu nchini  ni mengi  lakini leo nataka nizungumzie moja tu ambalo limekuwa changamoto kubwa  sana  kwa wasomi hawa  wa vyuo vikuu  na bado litaendelea kuwa changamoto yenye kuleta madhara makubwa  endapo serikali na mamlaka husika hazitawajibika ipasavyo kutafuta ufumbuzi na kulitatua kabisa tatizo hilo.

Swala la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini  limezua mjadala mzito sana  kwa wanafunzi  kwani  wasomi hao wamekuwa wakiiomba serikali iongeze fedha  za  mikopo  hususan fedha za kujkiimu wawapo vyuoni na pia  ada ikibidi..Kilio hiki cha wanachuo ni cha muda mrefu sana. na wengi   wamepoteza  masomo  kutokana na kushindwa kujikimu wenyewe kutokana na ugumu wa maisha  ambao kimsingi husababishwa na kupanda kwa gharama  za maisha .Bei ya bidhaa nchini inapanda kila kukicha na hivyo hata taasisi binafsi za elimu  zote pia inawalazimu kupandisha gharama za utoaji huduma.

Baada ya kilio cha muda mrefu  cha wasomi hawa kilichoambatana na  maandamano  na migomo kila kukicha serikali ikaanza walau kulifikiria na kuliangalia upya swala la mikopo na hatimaye kukiri kuwa  ni kweli ghrama za  maidha ya sasa si sawa na  kiwango cha fedha za kujikimu walichokuwa wanatoa  hadi hivi karibuni..Fedha ya kujikimu ya  mwanafunzi mmoja kwa siku ilikuwa ni shilingi za kitanzania elfu tano tu.Hivyo serikali kwa kuliona hilo,ikaamua kupandisha kiasi cha fedha hizo kutoka  shilingi elfu tano hadi elfu saba na  mia tano kwa siku ambapo imeongezeka  shilingi elfu mbili na mia tano tu ambayo imeanza kulipwa rasmi mwaka huu  wa masomo.

Hata hivyo  ongezelo la kutoka  shilingi elfu tano kwa siku hadi elfu  saba na mia tano halikuwa makubaliano kati  ya wanafunzi wa vyuo vikuu  kote nchini na serikali bali wasomi hao waliiomba serikali  kutokana na kupanda kwa gharama za maisha ongezeko la kutoka elfu tano hadi elfu kumi kwa siku.Hapa tunaona kuwa serikali haijatekeleza  wala  haijatoa suluhu bali imefanya kwa sehemu  tu kitu ambacho hakijawaridhisha wasomi hawa hata kidogo na ndio maana hata makala  za kuipongeza serikali  kwa utekelezaji huo hakuna!

Pamoja na kukubaliana na hali halisi ili kutopoteza wakati,wanafunzi wasomi  hawa wote wameamua kujikalia kimya huku wakijiliwaza  na kauli za wahenga kama vile, mvumiivu hula mbivu,na kwa ahadi za  seikali za tutafanya, basi wasomi hawa pia wanarejea  kwenye  kauli za wahenga kuwa  subira yavuta kheri.

Sasa tayari wanafunzi hawa wako vyuoni,  lakini badala ya kupungua maumivu ndio kwanza yameongezeka.Mamlaka iliyokabidhiwa dhamana ya  kushughulikia pesa za wanafunzi  ziwafikie kwa wakati yani Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu,(HSLB) inaonyesha kushindwa  kabisa kutekeleza jukumu lake,hali inayofunua hisia mpya kuwa kuna urasimu mkubwa ndani  ya chombo hicho cha serikali ambacho chenyewe pia kinatupa lawama kwa serikali  kwamba hatujapokea pesa kutoka serikalini.

Kutokana na kutokuwajibika kwa bodi ya mikopo na urasimu uliopo pamoja na rushwa iliyokithiri, serikali kutolichukulia uzito swala hili,madhara makubwa yanaendelea  kutokea,  ambapo mwaka huu takribani wanafunzi wapatao elfu kumi na nne wamekosa mkopo je watakwenda wapi wale watoto wa wakulima?

Kumeundwa bodi ndogo za mikopo vyuoni na serikali imetoa tamko kuwa  fedha za mikopo zitapelekwa vyuoni jambo ambalo ni kukiuka mkataba kati ya bodi ya mikopo na wanafunzi wanaoendelea  na  masomo kwa mwaka wa pili na kuendelea  kwa sababu  haukuwa hivyo.Fedha zilitakiwa zipelekwe  moja kwa moja kwenye akaunti za  wanafunzi wenyewe ili kuondoa  walau kwa sehemu tatizo la  ucheleweshaji wa fedha za kujikimu na ada kwa wanachuo hawa kwani baadhi ya vyuo wamekuwa wakichelewesha sana fedha za  kujikimu kwa wanafunzi.

Kumeibuka  hisia miongoni mwa wanafunzi wa baadhi ya vyuo  hapa nchini kuwa kuna vyuo  vikuu vinavyopewa kipaumbele  aidha kwa kuviogopa  au kwa namna yeyote ile ya kiupendeleo.Wasomi hawa wa wa vyuo baadhi wameilaumu mamlaka husika kwa kuchelewesha  fedha za vyuo vyao huku  huku wakihoji kwanini  vyuo vingine vipewe fedha kwa wakati na vingine visipewe kwa wakati?

Ni dhahiri kuwa serikali  kutokana  na kutojali na kutokulipa kipaumbele  swala  hili inashusha kiwango cha elimu nchini kwani migomo itaendelea kila kukicha na ndio maana hatukosei kabisa kusema kuwa  serikali itegemee migomo zaidi kwani  tatizo linazidi kuwa kubwa a badala ya kupungua.

Serikali haina budi  kulitizama upya  swala hili na kulitafutia ufumbuzi wa kudumu kama inavyohangaika na kuimarisha miundombinu ya barabara kuu nchini ambapo kwa kweli inafanya vizuri sana huko.

Aidha serikali   haina budi kuiwajibisha menejimenti ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu nchini na kuhakikisha kuwa  inaunda menejimenti madhubuti ambayo itafasnya kazi  kwa umakini  mkubwa na kwa haki huku mamlaka iliyokabidhiwa dhamana ya kuzuia  na kupambana na rushwa  ikiwa karibu kabisa na hivyo kuzuia urasimu na rushwa ambayo kimsingi ndio chanzo  cha matatizo.

                                                                     John Alex Mganga-0658385435

                                                                    E.mail-Johnmganga@yahoo.com.
                                                                            














No comments:

Post a Comment