.
Mojawapo ya nyumba zilizokumbwa na maji Tumaini.Na John Alex
Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo tofauti mkoani Iringa zimepelekea baadhi ya njia kadhaa za maeneo tofauti ya manispaa ya Iringa kupitika kwa shida kutokana na kufurika kwa mifereji na vijito vya maji hali inayosababisha miundombinu ya barabara na madaraja kupoteza ubora wake na kuanza kuharibika.
Hali hii imrjitokeza katika maeneo kadhaa yamanispaa ya Iringa ambapo baadhi ya maeneo hususan maeneo ya Semtema , Kihesa ,na maeneo ya chuo kikuu cha Tumaini njia zake kufurika maji wakati wa mvua hali inayopelekea wakazi wa maeneo hayo kupita kwa shida kwenye madaraja ambayo wakati wa mvua yalifurika maji.
Mvua zilizonyesha siku ya jumaatano zilifurisha mifereji na mito katika maeneo hayo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa sana kwa wakazi wa maeneo hayo kupita kwa shida kwenye madaraja ambayo yalijaa maji na kufanya miundombinu kuwa katika hatari ya kuharibika
Aidha mvua hizo zimehatarisha baadhi ya nyumba zilizojengwa pembezoni mwa mito na mifereji kwani maji yalikaribia karibu na kuta za nyumba zilizoko kwenye maeneo ya pembezoni mwa mifereji hiyo.
Wakazi wa Semtema wamesema kuwa mvua hizo zilizonza kunyesh a hivi kariibuni endapo zitaendelea kunyesha zitaharibu miundombinu ya barabara na madaraja kwani hayakujengwa kwa kiwango kinachotakiwa kuhimili mafuriko na mvua zilizokithiri.
Hata hivyo hali hiyo imejitokeza pia katika maeneo ya Zahanati maeneo ya Mwangingo ambapo baadhi ya nyumba ziliingia maji na kusababisha wasiwasi mkubwa kwa wakazi wenye nyumba zao maeneo pembezoni mwa mto kuhofia kukosa makazi baada ya kushuhudia maji yakiingia hadi ndani.
Wakazi wa maeneo hayo wamesema kuwa endapo mvua hizo zitaendelea kunyesha zitaleta maafa makubwa ikiwa ni pamoja na kupoteza maakazi kwa wananchi waliojenga nyumba zao pembezoni mwa mito.
Hata hivyo baadhi ya wakazi wa manispaa ya Iringa wameliambia kwanza jamii kuwa mvua zinazoendelea kunnyesha zitapnguza ukame na hivyo kufanya shughui za kilimo kuendelea vizuri lakini endapo zitaitiliza zinaweza ziksababisha hasara kwa mazao.
Mvua hizo zimesababisha uharibifu mkubwawa bostani za mbogamboga hususan kwa wakazi wa Tumaini ambao wamekuwa wakijihusisha na kilimo cha bostani za mbogamboga pembezoni mwa mto .
No comments:
Post a Comment