Na Solomon Ole Lekui
ALIYEKUWA
Muasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mohamed Bob
Makani amefariki dunia, maafisa wa Chadema wamethibitisha.
Makani
amefariki Dunia jioni ya leo jijini Dar kwenye hospital ya Aghakhan,
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amethibitisha hilo kwa njia ya simu
kutoka Kanda ya kusini walikokuwa wakifanya mikutano yao ya hadhara.
Mbowe amesema Marehemu Makani alikuwa akiugua kwa muda mrefu na kupelekwa hospitali mbalimbali kwa matibabu ikiwemo nje ya nchi.
Amesema mwili wa Marehemu umehamishiwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa hifadhi. Msiba upo nyumbani kwake Mbezi Beach jirani na Rainbow.Mbowe amesema Marehemu Makani alikuwa akiugua kwa muda mrefu na kupelekwa hospitali mbalimbali kwa matibabu ikiwemo nje ya nchi.
Watu wakiaga mwili wa marehemu Bob Makani
Rais
Jakaya Kikwete (katikati) akiwa na viongozi wakuu wa Chadema, Freeman
Mbowe (mwenyekiti) na Dk Willbroad Slaa (Katibu) kuuga mwili wa marehemu
Bob Makani, leo Karimjee.
Ukalale mahali pema mzee Bob Makani
No comments:
Post a Comment