Na Solomon Lekui
Picha
hii ya maktaba yetu, inamuonesha Profesa Peter Msolla (Mbunge wa Jimbo
la Kilolo) akiangalia jinsi wafanyabishara wa nyama ya nguruwe mjini
hapa wanavyofanya biashara yao
WAPENZI
wa ile nyama ya nguruwe maarufu kama Kitimoto inayoaminika kuongeza
kinga za mwili kwa watu walioshambuliwa na maambukizi ya Ukimwi kama
utaila sana, imepigwa marufuku kuuzwa mjini Iringa kuanzia leo.
Hatua
hiyo itakayowaacha mamia ya wafanyabiashara wake wakiathirika kiuchumi,
imekuja baada ya ugonjwa wa homa ya nguruwe kuripotiwa kuingia mjini
hapa.
Daktari
wa Mifugo wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Augustino Nyenza
amesema kuanzia leo machinjio zote za nguruwe zinatakiwa kufungwa
kwasababu ya tatizo hilo.
Amesema
tangu Mei 20 mpaka jana, ugonjwa huo ulikuwa umekwishauwa nguruwe 44
katika kata ya Mkwawa, huku uchunguzi uliofanywa ukioneshawa wengine
wengi wanasumbuliwa na ugonjwa huo.
Alisema
wakati halmashauri hiyo ikitangaza kuchinja na kuuza nyama ya nguruwe,
wananchi wanatakiwa kusubiri karantini kubwa ya wilaya.
“Tunaendelea kufanya mawasiliano kuhusu hali ya ugonjwa mjini Iringa ili karantini iweze kutangazwa rasmi,” alisema.
Alisema
karantini hiyo itazuia kuingiza, kutoa au kuuza nyama ya nguruwe mjini
hapa mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo baada ya ugonjwa huo
kudhibitiwa.
Hii ni mara ya pili kwa ugonjwa huo wa nguruwe kuingia mjini hapa katika kipindi cha mwaka mmoja na miezi mitatu iliyopita.
Mapema
mwezi Machi mwaka jana, ugonjwa huo uliingia mkoani Iringa ukitokea
mkoa jirani wa Mbeya ambako pia uliuwa idadi kubwa ya nguruwe.
Ugonjwa
huo uliingia mkoani Mbeya ukitokea katika wilaya ya Kalonga nchini
Malawi na baadae kuingia mkoani Iringa kwa kuanzia wilaya Ludewa
ulikouwa nguruwe 145 kati ya 716 katika kijiji cha Lupingu na Ntumbali.
Baada
ya kutangazwa kwa karantini, timu ya madaktari wa mifugo wa ofisi ya
kanda na halmashauri ya manispaa ya Iringa na Iringa Vijijini waliwauwa
kwa kuwachoma moto nguruwe 99 waliokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya
Sh Milioni 8.5, waliokamatwa wakisafirishwa kutoka Mbeya kwenda Dar es
Salaam.
No comments:
Post a Comment