Thursday, June 28, 2012

COCA COLA WAANDAA TUZO ZA WAANDISHI BORA WA MICHEZO WA COPA COCA COLA

    Na Consolata haule
              
     Coca-Cola Tanzania imetangaza kuanzisha tuzo kwa waandishi bora wa michuano ya soka ya vijana ya Copa Coca-Cola kwa nia ya kuwazawadia wanahabari wanaofanya kazi nzuri katika michezo,hivyo kuwa chachu ya mashindano ya Copa-Cola yenye lengo la kujenga
msingi wa maendeleo ya soka nchini Tanzania.
 
             Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam Meneja Masoko wa Coca Tanzania Salome Mabirizi alisema kuwa Coca-cola inatambua mchango mkubwa uliofanywa na waadishi wa habari kwa miaka mitano iliyopita katika kuwahamasisha kushiriki mashindano haya. Kuanzishwa kwa tuzo hizi ni njia moja wapo ya kuwashukuru waandishi wa habari kwa kazi nzuri ya kutangaza Coca-Cola.
 
           Alizitaja tuzo hizo kuwa ni mwandishi bora wa magazeti, mwandishi bora wa luninga, mwanahabari bora wa radio, mpiga picha bora (magazeti) na blogs bora, ambapo kila mshindi ataweza kuzawadiwa  thamani ya milioni 2 taslimu za kitanzania.

               Mchakato wa kuwapata washindi utafanywa kwa kushirikiana na Chama cha waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na Coca-Cola na tayari zoezi hilo limeshaanza tangu Jumapili juni 24 wakati fainali za Copa Coca-Cola Taifa zilipozinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam na  Fainali hizo zimepangwa kumalizika  Julai 15.
 
         Katibu Mkuu Msaidizi wa TASWA, George John aliwaambia waandishi wa habari kuwa kamati ya tuzo za Copa Coca-Cola itafanya kazi kwa kuzingatia vigezo ili kuweza kumpata mshindi anayestahili katika kila kundi lililotaja hapo juu.Pia amevitaja baadhi ya vigezo hivyo kuwa ni pamoja na stori au makala zinazohamasisha na kuwatia moyo vijana kuweza kuonyesha na kuendeleza vipaji vyao.
 
            Johan ameipongeza kampuni ya Coca-Cola kwa kushirikiana na Shirika la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuendesha mashindano hyo kwa nchi nzima kwa lengo la kuibua vipaji vya wanasoka chipukizi nchini Tanzania.
 
        Kiukweli Copa Caca_Cola imesaidia kubadili sura ya mpira wa miguu nchini Tanzania kwa kuwa chanzo cha kutegemewana wachezaji wenye vipaji wa kila timu za ligi kuu na timu za Taifa.  
NI mashindano pekee nchini ambayo huchezwa nchi nzima kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa yakishirikisha maelefu ya vijana kila mwaka ili kuwaendeleza vijana zaidi. 
 
        Coca-Cola imekuwa ikipeleka wachezaji bora wa Copa Coca-Cola kwenye kambi za kimataifa za mafunzo ya soka nchi za nje. Mnamo Mwaka 2007 na 2008 wachezaji bora wa Copa Coca-Cola walikwenda nchini Brazil na kuanzia 2008 hadi mwaka jana walipelekwa Afrika Kusini.
 
    Coca-Cola ni kampuni yenye historia ndefu ya kusaidia michezo ilianza kudhamini michezo ya olimpiki tangu 1928 na mpira wa miguu tangu 1930.  Kampuni ya Coca-Cola imekuwa ikidhamini Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) tangu 1974 na kuwa mdhamini rasmi wa FIFA tangu 1978 hadi sasa.
 
 
 
             Mkurugenzi mahusiano wa Coca Cola Kwanza( wa katikati )Bw. Evans Mlelwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za Coca Cola juu ya Tuzo kwa waandishi wa habari COPA COCA COLA,wa  kwanza kulia ni Katibu msaidizi  wa Taswa Bw. George John,kwa upande wa kushoto ni  Meneja Masoko wa Coca Cola Tanzania Bi.Salome Mabirizi.

No comments:

Post a Comment